Lugha Nyingine
Mlipuko wa Ebola wa DRC waelezwa bado ni dharura ya afya duniani wakati maambukizi yakizidi kuongezeka (2)
![]() |
| Wafanyakazi wa matibabu wakinyunyuzia dawa ya kuua vijidudu kwenye kituo cha matibabu ya Ebola, Beni, Jimbo la Kivu Kaskazini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Agosti 16, 2026. (Xinhua) |
KINSHASA - Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema Jumanne wiki hii kwamba mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) bado ni dharura ya afya ya umma inayofuatiliwa kimataifa (PHEIC), wakati janga hilo likizidi maambukizi 5,000, kuenea katika maeneo mapya na kusababisha mamlaka kutafuta chanjo na matibabu ya majaribio.
Mlipuko huu sasa ni mlipuko wa pili wa Ebola kwa ukubwa wake kuwahi kurekodiwa na unaenea kwa kasi zaidi kuliko yote iliyopita, Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema kwenye mkutano wa kamati ya dharura.
Hadi kufikia Jumapili, maambukizi 5,021 yaliyothibitishwa na vifo 2,378 vilikuwa vimeripotiwa kwenye kanda 55 za kiafya katika majimbo sita, huku kiwango cha vifo kikiwa asilimia 47.4, kwa mujibu wa hesabu ya hivi punde zaidi ya WHO.
Janga hilo, lililosababishwa na virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo, limepita mlipuko wa Ebola wa 2018-2020 mashariki mwa DRC, ambao hapo awali ulikuwa uliosababisha vifo zaidi nchini humo.
Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) vilisema Jumatatu kwamba mlipuko huo wa sasa unaua takriban mtu mmoja kila baada ya dakika 30 na una hatari ya kuwa janga la Ebola linaloua watu wengi zaidi kuwahi kurekodiwa duniani kote kama mwelekeo wake wa sasa hautabadilishwa haraka.
"Lazima tuseme kweli: janga hili liko mbali kutoka kuwa chini ya udhibiti," Tedros amesema. "Lilianza likiwa limetangulia kwa kiasi kikubwa mbele, na bado tunajitihada kulifikia."
Huku kukiwa hakuna chanjo au matibabu yaliyoidhinishwa yanayolenga mahsusi virusi hivyo vya Bundibugyo, mamlaka zinageukia zana za matibabu za majaribio na zilizobadilishwa matumizi ya awali.
“Chanjo mbili zilizoundwa mahsusi dhidi ya virusi hivyo vya Bundibugyo zimeingia katika majaribio ya binadamu,” Tedros amesema.
Jaribio la matibabu la PARTNERS linalofadhiliwa na WHO pia linatathmini dawa ya kupambana na virusi ya remdesivir, kingamwili ya monokloni ya majaribio ya MBP134 na mchanganyiko wake. Matokeo ya awali yanaweza kupatikana katika kipindi cha "karibu wiki tatu hadi nne," Waziri wa Afya wa DRC Roger Kamba amesema.
Watafiti pia wanaifanyia stadi dawa ya kumeza ya kupambana na virusi ya obeldesivir ili itumike kama kinga ya baada ya kuwa kwenye mazingira ya kuambukizwa.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




