Chama cha Wafanyakazi cha Brazil chamteua rasmi Lula kugombea muhula wa nne

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Agosti 03, 2026
Chama cha Wafanyakazi cha Brazil chamteua rasmi Lula kugombea muhula wa nne
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva akizungumza kwenye mkutano mkuu wa kitaifa wa Chama tawala cha Wafanyakazi, Sao Paulo, Brazil, Agosti 2, 2026. (Picha na Paulo Lopes/Xinhua)

RIO DE JANEIRO - Chama tawala cha Wafanyakazi cha Brazil (PT) Jumapili kimemteua rasmi Rais aliye madarakani Luiz Inacio Lula da Silva kuwa mgombea wake wa uchaguzi ujao wa rais anapotafuta muhula wa nne madarakani.

Kwenye mkutano mkuu wa kitaifa wa chama hicho mjini Sao Paulo jana Jumapili, wajumbe waliidhinisha rasmi tiketi ya kugombea urais inayowaweka pamoja Lula na Makamu wa Rais aliye madarakani Geraldo Alckmin wa Chama cha Kijamaa cha Brazil.

Rais wa PT Edinho Silva alitangaza kwamba chama hicho kimekamilisha usajili wake wa mgombea kwenye Mahakama ya Juu ya Uchaguzi.

Akihutubia mkutano huo, rais huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 80 amesema mafanikio ya utawala wake yatatumika kama msingi imara wa kampeni.

"Tunaweza kuwaonyesha kwa fahari watu wa kila mahali kile ambacho serikali kuu imefanikisha," Lula amesema.

Chini ya sheria za uchaguzi za Brazil, vyama vya siasa lazima vithibitishe wagombea wao ifikapo Agosti 5 na kukamilisha usajili rasmi ifikapo Agosti 15. Kampeni rasmi ya uchaguzi imepangwa kuanza Agosti 16.

Hapo awali Lula alihudumu mihula miwili mfululizo akiwa rais baada ya kushinda uchaguzi wa 2002 na 2006. Alirudi madarakani baada ya kushinda uchaguzi wa 2022 na kuanza muhula wake wa tatu Januari mwaka 2023.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha