Lugha Nyingine
Viwanda vya uundaji meli vya China vyaendelea kuongoza duniani katika mwaka 2025 (6)
![]() |
| Picha iliyopigwa Januari 13, 2026 ikionyesha meli ikiendelea kuundwa kwenye kiwanda cha Kampuni ya Usafirishaji wa Meli ya Cosco katika Mji wa Yangzhou, Mkoa wa Jiangsu, mashariki mwa China. (Picha na Meng Delong/Xinhua) |
Viwanda vya uundaji meli vya China vimedumisha nafasi kubwa zaidi kwenye soko duniani kutokana na viashiria vitatu vikuu vyake vya mwaka wa 16 kwa mfululizo katika mwaka 2025, takwimu zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Upashanaji wa Habari ya China siku ya Jumapili zinaonesha.
Katika mwaka 2025 uliopita, uundaji wa meli wa jumla wa China ulifikia tani milioni 53.69 za uzito (DWT) ongezeko lake lilifikia asilimia 11.4 ikilinganishwa na mwaka wa 2024 na kuchukua asilimia 56.1 ya jumla duniani.
Na oda mpya za viwanda hivyo vya China zilifikia DWT milioni 107.82 mwaka jana, ikichukua asilimia 69 ya sehemu ya soko la dunia.
Na hadi kufikia mwisho wa Desemba 2025, oda hodhi za viwanda hivyo vya China zilikuwa DWT milioni 274.42, ongezeko lake lilifikia asilimia 31.5 kuliko mwaka 2024 . Kiasi hicho kilichukua asilimia 66.8 ya sehemu ya soko la dunia.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




