

Lugha Nyingine
Kukarabati upya eneo la makazi kuboresha maisha ya wakazi wa Mji wa Fuzhou, China
Katika miaka ya hivi karibuni, Mji wa Fuzhou wa Mkoa wa Fujian, kusini mashariki mwa China umekuwa ukifanya juhudi kubwa za kutekeleza mipango ya kujenga upya maeneo ya makazi ya hali duni ya mjini.
Cangxia Xincheng ni eneo lililokuwa bovu lenye mazingira mabaya mjini humo Fuzhou, hivi sasa limebadilika kuwa eneo la makazi yanayofaa kuishi kwa watu baada ya kufanyiwa ukarabati na ujenzi wa ngazi ya juu kwa zaidi ya mwaka mmoja kuanzia mwezi Julai mwaka 2000. Septemba 2021, mpango wa duru mpya wa kukarabati na kujenga upya ulitekelezwa katika mji huo, ukiwekwa mkazo katika kufungamanisha hali ya utamaduni na historia na urahisi wa maisha katika mji huo. Miundombinu ya huduma mahsusi imejengwa kama vile kantini kwa wazee na vituo vya kulelea watoto. Kupitia ukarabati huo wa maeneo ya wakazi wa mjini, maisha ya watu yameboreshwa sana.
Wilaya ya Xuan’en yahimiza utalii wa usiku kando ya Mto Gongshui Katikati mwa China
Eneo la mtaa mkongwe lawa na ustawi kwa uvumbuzi wa kitamaduni na utalii mkoani Jiangxi, China
Mji wa Tianjin, China waharakisha ufungamanishaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi halisi
Ardhioevu yalinda spishi za ndege kutoka kwenye uwanda hadi mijini
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma