Kituo cha Anga ya Juu cha China chafanikisha kutoa mafunzo kutoka anga ya juu kwa mara ya pili (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 24, 2022
Kituo cha Anga ya Juu cha China chafanikisha kutoa mafunzo kutoka anga ya juu kwa mara ya pili
Wanafunzi wakitazama kwa kupitia video mafunzo ya sayansi yaliyotolewa na wanaanga wa China katika kituo kwenye anga ya juu katika Shule ya sekondari No.70 iliyoko Urumqi, Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uygur, Kaskazini Magharibi mwa China Machi 23, 2022.

Mchana wa Tarehe 23, Machi, mafunzo ya pili ya “Darasa la Tiangong” yalianza rasmi huku yakitangazwa moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti kwenye kituo cha anga ya juu cha China. Wanaanga watatu wa Shenzhou No.13 Zhai Zhigang, Wang Yaping, Ye Guangfu walitoa mafunzo hayo. Hii ni mara ya pili kwa kituo hiki cha China kutoa mafunzo kwenye anga ya juu, na pia ni mara ya tatu kwa wanaanga wa China kutoa mafunzo kutoka anga ya juu.

Wakati wa mafunzo hayo yaliyochukua dakika 45 hivi, wanaanga hao walishirikiana, wakionesha kwa udhahiri majaribio mbalimbali ya kiteknolojia katika mazingira yenye nguvu kidogo ya mvutano, kueleza kanuni za kisayansi za majaribio hayo, kuonesha baadhi ya vifaa vya kisayansi kwenye anga ya juu, na kujulisha mazingira ya kazi na maisha yao katika kituo hicho. Wakati wa muhadhara, wanaanga walifanya maingiliano na walimu na wanafunzi walioko duniani kwa kupitia video.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha