Lugha Nyingine
Marekani yaweka vikwazo vya viza kutokana na sera za Afrika Kusini kuhusu makabila na ardhi
(CRI Online) Septemba 17, 2026
Marekani imetangaza vikwazo vipya vya viza vinavyolenga raia fulani wa kigeni wanaohusishwa na sera za Afrika Kusini ambazo Marekani inasema zinabagua makabila madogo na zinaweza kuruhusu kunyang'anywa kwa ardhi bila fidia.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio alitangaza hatua hizo Jumanne, akisema kuwa serikali ya Afrika Kusini imeshindwa kushughulikia masuala yaliyowahi kuibuliwa na utawala wa Trump.
Vikwazo hivyo vitawahusu watu wanaochochea ubaguzi wa rangi, kuchochea vurugu au kuunga mkono kunyang'anywa kwa ardhi bila fidia. Hadi sasa hakuna watu binafsi waliotajwa wakati sera hiyo ilipotangazwa, na hatua hizo hazimaanishi marufuku ya jumla ya viza kwa raia wote wa Afrika Kusini.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



