Lugha Nyingine
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani wa Afrika wafunguliwa huko Cape Town
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani Afrika wa 2026 umefunguliwa mjini Cape Town, ambapo Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametoa wito wa kuharakisha utekelezaji na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji, ili kuubadilisha uwezekano wa haidrojeni ya kijani barani Afrika uwe ukuaji wa viwanda, usalama wa nishati, na maendeleo endelevu.
Mkutano huo wa siku mbili umeshirikisha wajumbe zaidi ya elfu moja kutoka nchi 17, wakiwemo maofisa wa serikali, wawekezaji, wataalamu wa nishati na viongozi wa sekta hiyo.
Kwenye hotuba iliyotolewa kwa niaba ya rais Ramaphosa, Waziri wa Umeme na Nishati Kgosientsho Ramokgopa amesema, Afrika imejiweka kwenye nafasi ya kuwa kituokikuu duniani cha haidrojeni ya kijani ikitaja nishati zake nyingi mpya, maliasili ya maji, pamoja na akiba kubwa ya madini muhimu.

people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



