Lugha Nyingine
Afrika Kusini yatoa wito wa kujenga mfumo jumuishi wa AI wa BRICS
Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametoa wito wa kujenga mfumo jumuishi, salama na wa ushirikiano kwa ajili ya matumizi ya AI kati ya nchi wanachama wa BRICS.
Shirika la Utangazaji la Afrika Kusini limenukuu hotuba ya Rais Ramaphosa kwenye mkutano wa kilele wa 18 wa BRICS uliofanyika huko New Delhi nchini India, akisema usimamizi wa binadamu lazima uendane na maendeleo ya AI.
Ameeleza kuwa uwezo wa modeli za AI unazidi kuwa na nguvu na unaleta mabadiliko ya kasi kwenye karibu sekta zote za uchumi na jamii, na kuweza kufungua zama mpya ya tija na maendeleo ya binadamu, ambapo mfumo husika unatakiwa kuungwa mkono na "kanuni za udhibiti wa binadamu zenye maana, utoaji ripoti wa lazima kuhusu matukio makubwa, hatua za ulinzi zinazoimarishwa kuendana na ukuaji wa uwezo, na uwekezaji sambamba katika uwezo wa AI wa kitaifa kwa nchi zinazoendelea."
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



