Lugha Nyingine
Kauli za Trump kuhusu kuungana kwa Ireland zazua upingaji kutoka Uingereza

Watu wakitembea kutoka nje ya tawi la Benki ya Ireland jijini Dublin, Ireland, tarehe 1 Machi 2021. (Xinhua)
LONDON - Kauli za Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu kuungana kwa Ireland na Ireland Kaskazini ya Uingereza zimezua upingaji mkali kutoka Uingereza.
Kwenye ziara ya siku mbili nchini Ireland mwishoni mwa wiki, Trump alisema siku ya Jumamosi kuwa "angependa kuona" kuungana kwa Ireland na Ireland Kaskazini.
"Rais Trump anatoa kauli bila kujali athari kama kawaida yake, sawa tu na alivyofanya na Greenland na suala la Canada kuwa jimbo la 51," amesema kiongozi wa Chama cha Conservative, Kemi Badenoch, katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa X siku ya Jumamosi.
Ameongeza kuwa "Ireland Kaskazini ni sehemu ya Uingereza."
"Sikubaliani na Rais Trump," amesema kiongozi wa chama cha Reform UK, Nigel Farage, katika ujumbe wake kwenye mtandao wa X siku hiyo hiyo, "Ireland Kaskazini ni sehemu ya kujivunia na isiyoweza kutengwa ya Uingereza."
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



