Lugha Nyingine
Trump atangaza mazungumzo na Iran leo Jumatatu
"Kuna makubaliano kuhusu (Mlango-Bahari wa) Hormuz, na kisha kutakuwa na makubaliano kuhusu nyuklia, au unaweza kuyaita kuondoa silaha za nyuklia kwa Iran," Trump amewaambia waandishi wa habari ndani ya Air Force One jana Jumapili wakati akiwa njiani kuelekea Joint Base Andrews.
Huku akidai kwamba Iran pia imeiomba Marekani kusitisha mashambulizi yaliyopangwa, Trump amesema kwamba "sasa tunachofanya ni kuzungumza nao kupitia mazungumzo."
Mwanamfalme Mteule wa Saudi Arabia ambaye pia ni Waziri Mkuu Mohammed bin Salman Al Saud alizungumza kwa njia ya simu na Trump siku ya Jumamosi na "kueleza hali ya wasiwasi na kuomba ufafanuzi" kuhusu mpango uliopendekezwa wa kuchukua hatua dhidi ya Iran, afisa wa Marekani alikiambia chombo cha habari cha Axios.
Pakistan, Qatar, UAE, Uturuki na nchi zingine pia zimetoa wito kwa Marekani na Iran kupunguza kupamba moto kwa mivutano na kuepuka mgogoro zaidi.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



