Li Qiang ampongeza Andy Burnham kwa kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza

(CRI Online) Julai 21, 2026

Waziri Mkuu wa China Li Qiang amemtumia salamu za pongezi Andy Burnham jana Jumatatu kwa kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza.

Li amesema China na Uingereza zote ni wajumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na nchi zenye uchumi mkubwa duniani, na ameongeza kusema kuwa mazungumzo na ushirikiano imara zaidi si tu vinasukuma mbele maendeleo ya nchi hizo mbili, bali pia vinachangia utulivu mkubwa zaidi kwenye amani duniani.

Li ameeleza utayari wake wa kushirikiana na Burnham kuimarisha mazungumzo, kuzidisha kuaminiana, kupanua mabadilishano na ushirikiano, na kusukuma mbele uhusiano wa washirika wa kimkakati kwa pande zote kati ya China na Uingereza, ili kuleta manufaa zaidi kwa nchi hizo mbili na wananchi wao.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha