Lugha Nyingine
Maofisa wataka unyumbufu wa kifedha wakati Afrika ikikabiliwa na pengo kubwa la bima
Maofisa na watunga sera wametoa wito wa hatua za dharura kuimarisha unyumbufu wa kifedha na kulinda nchi za Afrika dhidi ya hatari zinazoongezeka, wakati bara hilo likikabiliwa na pengo kubwa la bima.
Wakizungumza katika mkutano wa mwaka wa ZEP-RE 2026, ulioandaliwa na Kampuni ya PTA Reinsurance, taasisi ya kitaalamu ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) na serikali ya Rwanda, uliofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kigali, watunga sera na wadau wa biashara wameonya kuwa mamilioni ya watu na makampuni yako hatarini kwa mishtuko inayotokana na majanga ya asili na mvurugiko wa kiuchumi.
Mkutano huo ulihusisha majadiliano ya ngazi ya juu yaliyolenga ufadhili wa tishio la majanga, ikiwemo ulinzi wa mali za umma na utulivu wa kifedha, na bima jumuishi.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



