China yahimiza mapambano yasimamishwe mashariki mwa DRC

(CRI Online) April 17, 2026

Mwakilishi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa Balozi Sun Lei amehimiza jumuiya ya kimataifa kuyafanya mapambano yasimamishwe mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Akihutubia mkutano wa wazi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya eneo la Maziwa Makuu, Balozi Sun amesema, jamii ya kimataifa lazima ihimize pande zote zinazopambana kutekeleza azimio husika la Baraza la Usalama, kuhakikisha ahadi za kusimamisha mapambano zinatekelezwa kivitendo, na kuepukana na hatua zinazoweza kuongeza mvutano.

Pia amesisitiza kuwa China iko tayari kuendelea kushirikiana na pande zote pamoja na nchi za eneo hilo, kuimarisha ushirikiano wa kunufaishana na nchi za eneo hilo, na kusaidia eneo hilo kutimiza amani ya kudumu na maendeleo yenye ustawi.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha