Wataalamu wa Zambia wasema sera ya ushuru sifuri ya China itachochea maendeleo ya Afrika

(CRI Online) April 17, 2026

Wataalam kutoka nchini Zambia wamesema, sera ya ushuru sifuri ya China kwa bidhaa zinazotoka nchi 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia na China itaimarisha kidhahiri maendeleo ya nchi za Afrika na kuchochea mabadiliko katika viwanda.

Katibu mkuu wa Shirikisho la Urafiki la Zambia na China Fredrick Mutesa ameliambia Shirika la Habari la China Xinhua kwamba, hatua hiyo itawakilisha fursa kubwa za maendeleo kwa nchi za Afrika, na kuzitaka nchi hizo kufuatilia kwa karibu mahitaji ya kuingia katika soko la China kama zinataka kufaidika zaidi. Pia amependekeza mageuzi katika mifumo ya elimu katika nchi husika ili kuzalisha ujuzi unaoendana na mahitaji ya uchumi wa dunia, na kuongeza kuwa, ujuzi katika maendeleo ya kidijitali na teknolojia rafiki wa mazingira vinapaswa kuwa sehemu ya mageuzi hayo.

Kelvin Chisanga, mchumi kutoka Zambia, amesema sera hiyo itaimarisha ushindani wa bidhaa za Afrika, kufungua fursa mpya kwa sekta kama madini, kilimo na utengenezaji.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha