Wanaharakati wa Afrika wakutana Kenya kutoa wito wa haki ya mabadiliko ya tabianchi

(CRI Online) April 17, 2026

Wanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi barani Afrika wamekutana Nairobi, mji mkuu wa Kenya, jana Alhamis, kujadili msimamo wa pamoja kuhusu ufadhili wa mageuzi ya kijani.

Akizungumza katika mkutano huo, mwenyekiti wa Kundi la Wataalam wa Afrika la Majadiliano kuhusu mabadiliko ya Tabianchi Nana Antwi-Boasiako Amoah amesema, majadiliano hayo yatatoa kipaumbele katika sekta za kilimo, usalama wa chakula, usawa wa jinsia na ufadhili wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Amesema wakati majadiliano ya kimataifa yanayofanyika chini ya mfumo wa Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa yakiendelea, kuna haja ya dharura ya kuimarisha utekelezaji wa hatua za mabadiliko ya tabianchi, hususan ndani ya mifumo ya sekta ya kilimo na chakula.

Amesema kilimo lazima kipewe umuhimu mkubwa katika majadiliano ya kimataifa kwa kuwa kinadumu kuwa kipaumbele kwa Afrika kutokana na nafasi yake katika maendeleo ya uchumi, pato la jumla la ndani, ajira na usalama wa chakula.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha