Rais wa Marekani asema nchi hiyo na Iran huenda zikafanya mazungumzo ya moja kwa moja wikiendi hii

(CRI Online) April 17, 2026

Rais Donald Trump wa Marekani jana amesema, Marekani huenda itafanya mazungumzo ya moja kwa moja na Iran wikiendi hii, na kama nchi hizo mbili zikifikia makubaliano ya amani, atazingatia kwenda Pakistan na kuyasaini makubaliano.

Rais Trump amesema makubaliano ya amani yatailetea Marekani "Mafuta bila malipo na Mlango wa Hormuz". Vilevile amesisitiza kuwa Iran haipaswi kuwa na silaha za nyukilia, na Iran imekubali kukabidhi uranim iliyosafishwa kwa Marekani.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha