Tanzania yatarajia kupokea watalii zaidi kutoka China

(CRI Online) April 16, 2026

Tanzania imerejea tena utayari wake wa kuvutia watalii zaidi kutoka China wakati vituo vya utalii vya Afrika vikiongeza juhudi kutumia vizuri fursa inayotokana na soko kubwa la watalii wa kigeni.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) jana imesema, ahadi hiyo imetolewa wakati wa majadiliano ya ngazi ya juu yaliyopewa jina la “Utalii wa Nje wa China na Vituo vya Afrika” yaliyofanyika katika Mkutano wa Afrika wa Soko la Utalii Duniani wa 2026 mjini Cape Town, Afrika Kusini, na kuwakutanisha wadau wa sekta hiyo waliotafiti mikakati ya kuiweka Afrika kama kivutio cha watalii kutoka China.

Akiwakilisha Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa TTB Ephraim Mafuru amesema, nchi hiyo imejiandaa vema kuvutia watalii kutoka China, na imeendeleza uelewa wa kina wa matakwa yao na matarajio yao.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha