Watu 7 wafariki kufuatia maporomoko ya udongo mashariki mwa DRC

(CRI Online) Machi 04, 2026

Watu saba wamefariki na wengine hawajulikani walipo baada ya maporomoko ya udongo kutokea jana Jumanne katika eneo la uchimbaji madini la Rubaya, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Machimbo hayo ya Rubaya yaliyoko Jimbo la Kivu Kaskazini ni chanzo muhimu cha madini ya coltan duniani na tangu mwaka 2024, yamekuwa yakidhibitiwa na waasi wa kundi la M23.

Mwezi Januari mwaka huu, wachimba madini 200 walifariki baada ya mashimo kadhaa ya migodi kuporomoka kwenye machimbo ya coltan ya Rubaya.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha