Lugha Nyingine
Mkutano wa Nishati wa Afrika 2026 wafunguliwa mjini Cape Town kwa kuweka mkazo katika mageuzi ya kiviwanda

Waziri wa Umeme na Nishati wa Afrika Kusini, Kgosientsho Ramokgopa, akitoa hotuba ya ufunguzi kwenye Mkutano wa Nishati wa Afrika 2026 (Africa Energy Indaba 2026) mjini Cape Town, Afrika Kusini, Machi 3, 2026. (Picha na Xabiso Mkhabela/Xinhua)
CAPE TOWN – Mkutano wa 28 wa Nishati wa Afrika 2026 (Africa Energy Indaba 2026) umefunguliwa rasmi jana Jumanne mjini Cape Town kwa kujikita katika kusukuma mbele mabadiliko ya viwanda ya Afrika kupitia mageuzi ya nishati, upanuzi wa miundombinu, na mafungamano ya kikanda.
Mkutano huo unaofanyika kuanzia Jumanne hadi Alhamisi kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Cape Town chini ya kaulimbiu isemayo "Kuwasha Mapinduzi ya Umeme," unawaleta pamoja viongozi wa serikali, mashirika ya kutoa huduma za umeme, wasimamizi, wawekezaji, na watendaji wa sekta ili kuharakisha utekelezaji, kuendana kwa miundombinu, na uhamasishaji wa uwekezaji.
Katika hotuba yake ya ufunguzi, Waziri wa Umeme na Nishati wa Afrika Kusini, Kgosientsho Ramokgopa, amesema mfumo wa nishati duniani unabadilishwa na ushindani wa siasa za kijiografia na sera za viwanda.
"Tunakusanyika hapa katika wakati wa matokeo makubwa ya kihistoria," amesema, akiongeza kuwa "nishati imekuwa usanifu wa kimya wa nguvu duniani.
Ramokgopa amesema kwamba wakati Afrika ni kitovu cha kimuundo cha mpito wa nishati duniani kwa sababu ya maliasili zake muhimu za madini, ni lazima iepuke kurudia mtindo wa kusafirisha malighafi nje bila kujenga minyororo ya thamani ya ndani.
Ratiba ya mkutano huo wa siku tatu inajumuisha mazungumzo ya mezani ya mawaziri na mazungumzo ya viongozi wa nishati, pamoja na majukwaa mahsusi na shughuli za pembezoni zanazohusu sehemu muhimu za mnyororo wa thamani ya umeme na nishati.
Vikao vya faragha vya kukutanisha wadau wa uwekezaji vitafanyika kwa lengo la kuunganisha wafadhili wa miradi na wawezeshaji fedha, wakati huohuo shughuli za maonyesho na za kujenga mitandao – zikiwemo za warsha, semina, na mapokezi ya kipekee -- yanawezesha ushiriki wa kimkakati.
Ajenda ya 2026 inajikita katika kuimarisha masoko ya umeme ya kikanda na biashara ya kuvuka mipaka, kufungua maendeleo ya gesi hadi umeme na gesi ya ndani, kuharakisha usambazaji na upanuzi wa gridi ya taifa, kuhamasisha fedha mchanganyiko na mtaji binafsi, na kusukuma mbele uhakika wa usimamizi na utayari wa uwekezaji.
Kwa mujibu wa mratibu, mkutano huo umeleta wajumbe 1,662 wa mkutano kutoka nchi 37 za Afrika, wakiwemo mawaziri 15 wa nishati wa Afrika na wazungumzaji wataalamu 173. Watembeleaji zaidi ya 4,300 wanatarajiwa kutembelea Maonyesho ya Mkutano huo wa Nishati wa Afrika yanayofanyika sambamba na mkutano mkuu.

Watu wakihudhuria semina kwenye Mkutano wa Nishati wa Afrika 2026 mjini Cape Town, Afrika Kusini, Machi 3, 2026. (Xinhua/Wang Lei)

Watu wakihudhuria semina kwenye Mkutano wa Nishati wa Afrika 2026 mjini Cape Town, Afrika Kusini, Machi 3, 2026. (Xinhua/Wang Lei)

"Tamasha la Maolong" la kabila la Wayilao lasherehekewa kwa ngoma ya dragoni mkoani Guizhou, China

Mji mkongwe wa Wuzhen, China wazindua shughuli mbalimbali wakati wa Mwaka Mpya wa Jadi wa China

Hong Kong Yasherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa Farasi wa China kwa Maonyesho ya Fataki

Ufunguzi ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Milan-Cortina mwaka 2026
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma