China yatoa wito wa kurudi kwenye mazungumzo juu ya suala la nyuklia la Iran

(CRI Online) Machi 04, 2026

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Mao Ning amesema China inatoa wito wa kukomeshwa kwa operesheni za kijeshi na kurudi kwenye meza ya mazungumzo juu ya suala la nyuklia la Iran mapema iwezekanavyo.

Kauli hiyo ya Mao ameitoa jana Jumanne kwenye mkutano na waandishi wa habari. Kabla ya hayo, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) Dr. Rafael Mariano Grossi alisema juzi Jumatatu kwamba hakuna ushahidi kuwa Iran imekuwa ikiendesha mpango wa "kimfumo" wa silaha za nyuklia.

Mao amesisitiza kuwa China ina wasiwasi mkubwa kuhusu Marekani kuishambulia Iran wakati wa mchakato wa mazungumzo, ambayo inakiuka sheria za kimataifa na utaratibu wa kawaida unaoongoza uhusiano wa kimataifa, na ambayo imesababisha kupamba moto kwa ghafla kwa mivutano katika eneo la Mashariki ya Kati.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha