Lugha Nyingine
Ongezeko la Uchumi wa Hong Kong lakadiriwa kufikia asilimia 2.5 hadi 3.5 mwaka 2026

Paul Chan, mkuu wa ofisi kuu ya fedha ya Serikali ya Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China, alitangaza bajeti ya 2026-27 ya Hong Kong, kusini mwa China, Februari 25, 2026. (Xinhua/Zhu Wei)
HONG KONG –Paul Chan, mkuu wa ofisi kuu ya fedha ya Serikali ya Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China, amesema Jumatano kuwa kwa mujibu wa tathmini ya hali ya hivi sasa ya uchumi wa dunia na wa ndani ya China, ongezeko la uchumi wa Hong Kong linakadiriwa kufikia asilimia 2.5 hadi asilimia 3.5 katika mwaka 2026.
Chan alipotangaza bajeti ya mwaka wa 2026-2027 ya Hong Kong alisema kuwa, “sehemu mbalimbali nchini China zitakuwa injini muhimu za msukumo wa uchumi wa kikanda na dunia, na kutoa uungaji mkono mkubwa kwa Hong Kong”.
“China itatekeleza sera za jumla za kuhimiza juhudi zaidi mwaka huu, ikipanua mahitaji ya ndani na kusukuma mbele maendeleo ya sifa bora kwa hatua madhubuti, huku ikidumisha ongezeko la uchumi linalofaa,” Chan amesema, na kuongeza kuwa, hali hii itajenga mazingira mazuri kwa ongezeko la uchumi wa Hong Kong.
Chan amesema, kutokana na uhimizaji wa uwekezaji katika sekta ya teknolojia ya AI na teknolojia nyingine mpya, mahitaji ya bidhaa husika yanaendelea kuchangia upanuzi wa biashara barani Asia.
Amekadiria kuwa, mauzo ya nje ya bidhaa za Hong Kong yatadumisha ongezeko zuri na mahitaji ya ndani yataongezeka kwa hatua madhubuti mwaka huu. Na kuongezwa kwa imani juu ya biashara, pamoja na matarajio ya kupunguzwa kwa viwango vya riba, kutachochea ongezeko kwenye masoko ya mali na uwekezaji.
Chan amesema, kiasi cha mfumuko wa bei wa sehemu inayoweza kudhibitiwa cha Hong Kong na kiasi cha jumla cha mfumuko wa bei cha Hong Kong vinakadiriwa kufikia asilimia 1.7 na asilimia 1.8 katika mwaka 2026, mtawalia.
Amesema, kuanzia 2027 hadi 2030, wastani wa ongezeko halisi la uchumi wa Hong Kong unakadiriwa kufikia asilimia 3 kwa mwaka, na wastani wa mfumuko wa bei kwenye sehemu ya uchumi inayoweza kudhibitiwa utafikia asilimia 2 kwa mwaka.
Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa ongezeko la uchumi wa Hong Kong lilifikia asilimia 3.5 katika mwaka 2025, ikimaanisha mwaka wa tatu mfululizo wa kukua kwa uchumi.

Paul Chan, mkuu wa ofisi kuu ya fedha ya Serikali ya Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong wa China, akitangaza bajeti ya 2026-27, Hong Kong, kusini mwa China, Februari 25, 2026. (Xinhua/Zhu Wei)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



