

Lugha Nyingine
China siku zote imekuwa ikichukua hatua madhubuti kuendeleza maendeleo ya kimataifa: Msemaji
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Lin Jian amesema, China siku zote imekuwa nchi inayochukua hatua madhubuti katika kuendeleza maendeleo ya kimataifa, na inapenda kushirikiana na pande zote kuhimiza ustawi na maendeleo ya pamoja duniani.
Akijibu swali kutoka kwa mwandishi wa habari kwenye mkutano na waandishi wa habari jana Alhamisi mjini Beijing, Bw. Lin amesema, janga la maendeleo limekuwa ni changamoto halisi inayozikabili nchi zote, na China siku zote imekuwa ikichukua hatua thabiti kuendeleza maendeleo ya kimataifa.
Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulitoa ripoti ya tathmini ya utekelezaji wa Ajenda ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030, ikionyesha kuwa karibu nusu ya malengo yamepiga hatua polepole, na asilimia 18 ya malengo yamerudi nyuma.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amesema, dunia inakabiliwa na "dharura ya maendeleo", lakini malengo hayo bado yanaweza kufikiwa, endapo pande zote zinaweza kuchukua hatua za haraka, za pamoja na zisizo za kuyumbayumba.
Wilaya ya Xuan’en yahimiza utalii wa usiku kando ya Mto Gongshui Katikati mwa China
Eneo la mtaa mkongwe lawa na ustawi kwa uvumbuzi wa kitamaduni na utalii mkoani Jiangxi, China
Mji wa Tianjin, China waharakisha ufungamanishaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi halisi
Ardhioevu yalinda spishi za ndege kutoka kwenye uwanda hadi mijini
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma