

Lugha Nyingine
Chama tawala nchini Zambia chasifu ziara yake nchini China
Chama tawala nchini Zambia United Party for National Development (UPND) kimeelezea ziara yake ya hivi karibuni nchini China kwamba ni uzoefu wa thamani wa kujifunza, si tu kuimarisha uhusiano na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), bali pia kwa kuchangia maendeleo ya taifa ya Zambia.
Mkurugenzi wa Habari wa UPND Mark Simuuwe amesema, majadiliano yaliyofanyika na maofisa wa CPC yalikuwa ni muhimu katika kuongeza nguvu ya uhusiano kati ya vyama hivyo viwili vya kisiasa na katika kutafiti mikakati ya maendeleo inayoweza kuwa na manufaa kwa Zambia.
Amesisitiza kuwa Zambia ina mengi ya kujifunza kutoka njia ya maendeleo ya China, hususan mkakati wa China wa kuondokana na umasikini kama mfano ambao Zambia inaweza kuutumia katika kukabiliana na changamoto zake za umasikini.
Wilaya ya Xuan’en yahimiza utalii wa usiku kando ya Mto Gongshui Katikati mwa China
Eneo la mtaa mkongwe lawa na ustawi kwa uvumbuzi wa kitamaduni na utalii mkoani Jiangxi, China
Mji wa Tianjin, China waharakisha ufungamanishaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi halisi
Ardhioevu yalinda spishi za ndege kutoka kwenye uwanda hadi mijini
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma