

Lugha Nyingine
FOCAC inaendeleza ushirikiano kati ya Afrika na China katika ujenzi wa miundombinu
Waziri wa Kazi na Uchukuzi wa Uganda, Katumba Wamala amesema, Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) linalotimiza miaka 25 mwaka huu, limeibuka na kuwa jukwaa muhimu kwa nchi za Afrika kutoa sauti ya vipaumbele vyao vya maendeleo na mikakati inayoendana na China kwa ukuaji wa pamoja.
Akizungumza hivi karibuni katika mahojiano na Shirika la Habari la China, Xinhua yaliyofanyika Wilaya ya Kayunga, katikati ya Uganda, Waziri huyo amesema FOCAC imeziwezesha nchi nyingi za Afrika kuendeleza miradi ya nishati muhimu na miundombinu ya uchukuzi kwa kuungwa mkono na China.
Amesema Uganda imefaidika sana na ushirikiano unaotokana na FOCAC, akitolea mfano upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe, na ujenzi wa Barabara Kuu ya Kampala – Entebbe.
Wilaya ya Xuan’en yahimiza utalii wa usiku kando ya Mto Gongshui Katikati mwa China
Eneo la mtaa mkongwe lawa na ustawi kwa uvumbuzi wa kitamaduni na utalii mkoani Jiangxi, China
Mji wa Tianjin, China waharakisha ufungamanishaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi halisi
Ardhioevu yalinda spishi za ndege kutoka kwenye uwanda hadi mijini
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma