UN na AU wazitaka pande zinazozozana nchini Sudan Kusini kufanya mazungumzo

(CRI Online) Mei 09, 2025

Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mataifa (UN), na waangalizi wa amani nchini Sudan Kusini wametoa wito kwa viongozi wa nchi hiyo kusitisha uhasama na kuanza tena kufanya mazungumzo haraka ili kuendeleza utekelezaji wa makubaliano ya amani.

Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa mjini Juba nchini Sudan Kusini, Ujumbe wa AU nchini Sudan Kusini, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, Mamlaka ya Kiserikali kwa ajili ya Maendeleo, Jumuiya ya Afrika Mashariki, na Kamisheni Mpya ya Pamoja ya Ufuatiliaji na Tathmini, ambayo inafuatilia utekelezaji wa amani, wameelezea wasiwasi wao kuhusu kuzorota kwa kasi kwa hali ya kisiasa na usalama kote Sudan Kusini.

Ujumbe huo umesema mazungumzo jumuishi ya kisiasa yanaweza kufikiwa kupitia kuachiliwa kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar na maafisa wengine na wanachama wa upinzani walioko kizuizini kwa sasa, na pia kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuitisha tena na kufadhili taasisi na taratibu zilizowekwa chini ya makubaliano ya amani.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha