Mchanuo wa Maua ya Rapa yenye Rangi ya Dhahabu Wachochea Utalii wa Wilaya ya Tongzi, China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 24, 2025

Kuanzia Jumamosi, Machi 24 maua ya rapa katika mji wa Guangcang, Wilaya ya Tongzi, Mkoa wa Guizhou nchini China, yalifikia mchanuo wao kamili. Shamba kubwa la rapa lenye ukubwa wa ekari elfu moja limegeuka kuwa bahari ya rangi ya dhahabu yenye uzuri wa aina yake, likivutia watalii kujichangamanisha katika uzuri wa msimu wa mchipuko.

Katika miaka ya hivi karibuni, Wilaya hiyo ya Tongzi imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika uendelezaji utalii wa vijijini. Imechochea kwa kina rasilimali zake za utalii wa vijijini na kuandaa kwa umakini matukio mbalimbali kama vile "Tamasha la Kijiji". Hili limehimiza kwa ufanisi mfungamano wa kina wa utamaduni na utalii, ukitoa msukumo wa kila mara kwa ustawishaji wa vijiji.

Mwaka 2024, Tongzi ilipokea jumla ya watalii zaidi ya milioni 16.89, ikifikia mapato jumuishi ya utalii ya Yuan bilioni 19.39.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha